Ligi Kuu ya NBC mzunguuko wa 26 , mechi tatu leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th June 2026


Ligi Kuu ya NBC mzunguuko wa 26 , mechi tatu leo

Baada ya takribani wiki mbili za mapumziko ya kalenda ya FIFA, Ligi Kuu ya NBC inarejea leo mzunguuko wa 26 kwa mechi tatu kupigwa.

Fountain Gate watakuwa wenyeji wa Azam Fc mchezo utakaopigwa saa 10 uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha wakati Coastal Union wakiwakaribisha Namungo Fc katika mchezo mwingine utakaokuwa unapigwa muda huo kwenye uwanja wa Mkwakwani mkoani Tanga.

Mchezo utakaohitimisha ratiba ya leo ni kati ya KMC dhidi ya TRA United uwanja wa KMC Complex.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.